Tuesday, 6 July 2010

clouds TV yazindua logo yake rasmi usiku wa kuamkia leo

Sehemu ya Logo ilivyokuwa ikionekana kwenye scrini wakati wa uzinduzi
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Clouds Entertainment Joseph Kusaga akizungumza jambo usiku wa kuamkia leo wakati wa uzinduzi maalumu wa nembo a.k.a Logo ya Clouds TV pamoja na mchakato rasmi wa kuzianza mbio za tamasha la Fiesta 2010 lenye kauli mbiu ya Jipanguse Kiserengeti rrhaaaa raaaahhh.,Tamasha hilo linaanza kurindima kesho mkoani Morogoro katika uwanja wa Jamhuri,kiingilio kimepangwa kuwa ni buku mbili kwa kila kichwa.Mdhamini mkuu wa tamasha hilo ni kampuni ya bia ya Seregeti .
Bw.Joseph Kusaga akiwashukuru wageni waalikwa kwa kufika kwao kwenye uzinduzi huo usiku wa kuamkia leo katika kiota cha maraha cha Bilicanas,wengineo pichani ni baadhi ya waliofanikisha uzinduzi wa nembo ya Clouds TV.
Mmoja wa wakurugenzi wa Clouds Entertainment Ruge Mutahaba akimkaribisha Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Clouds Entertainment Joseph Kusaga kuzungumza machache mbele ya wageni waalikwa katika uzinduzi huo.
Mmoja wa viongozi waandamizi wa Clouds Entertainment,Sheba Kusaga akiwashukuru wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye hafla fupi ya uzinduzi maalumu wa nembo a.k.a Logo ya Clouds TV pamoja na mchakato rasmi wa kuzianza mbio za tamasha la Fiesta 2010.

Baadhi ya watangazaji wa Clouds TV wakitambulishwa mbele ya wageni waalikwa
Hussein Machozi akiwatumbuiza wageni waalikwa.
Msanii Keisha kutoka kundi la Tip Top Conections
Lina kutoka THT
Diamond na full swagga jukwaani
Diamond akiimba wimbo wake wa mbagala mbele ya wageni waalikwa
Baadhi ya wageni waalikwa kwenye usiku wa uzinduzi maalumu wa nembo a.k.a Logo ya Clouds TV pamoja na mchakato rasmi wa kuzianza mbio za tamasha la Fiesta 2010.
Baadhi ya wasanii kutoka THT wakitumbuiza kwa umahiri mkubwa wageni waalikwa waliofika kwenye maalumu wa nembo a.k.a Logo ya Clouds TV pamoja na mchakato rasmi wa kuzianza mbio za tamasha la Fiesta 2010.
Mpiga Picha wa Clouds TV akirekodi tukio la mahojiono mafupi ya wageni waliokuwa wakiwasili kwenye uzinduzi huo wa wa uzinduzi maalumu wa nembo a.k.a Logo ya Clouds TV pamoja na mchakato rasmi wa kuzinaza mbio za tamasha la Fiesta 2010 lenye kauli mbiu ya Jipanguse Kiserengeti rrhaaaa raaaahhh,kushoto ni Mtangazaji Zamaradi Mketema na mgeni mualikwa.
Wapo tayari kwa kulianzisha libeneke .
Wana wa Clouds TV wakishoo love mbele ya camera ya Jiachie kabla uzinduzi kuanza rasmi
Mtangazaji wa Cloods FM kupitia kipindi cha Ala za Roho Loveness Love pamoja na mtangazajiwa Clouds FM/TV Antonio Nugaz.
Kutoka kulia ni mmoja wa Wakurugenzi wa Clouds Entertainment Ruge Mutahaba,Hk mmoja wa wapiga picha Clouds TV,Ankal Anwar wa 2 Eyes Productions pamoja na msanii wa muziki wa kizazi Diamond wakiwa wamenaswa na Camara ya Jiachie usiku wa kuamkia leo wakati wa uzinduzi maalumu wa nembo a.k.a Logo ya Clouds TV pamoja na mchakato rasmi wa kuzinaza mbio za tamasha la Fiesta 2010 lenye kauli mbiu ya Jipanguse Kiserengeti rrhaaaa raaaahhh.
Baadhi ya crew ya Clouds TV wakiwa mzigoni tayari kuyanasa matukio yatakayokuwa yakijiri kwa usiku huo uliofanyika ndani ya kiota cha maraha Club Billicanas.
Wadau wa 2 Eyes Productions wakiwa bize mzigoni usiku wa kuamkia leo wakati wa uzinduzi maalumu wa nembo a.k.a Logo ya Clouds TV pamoja na mchakato rasmi wa kuzinaza mbio za tamasha la Fiesta 2010 lenye kauli mbiu ya Jipanguse Kiserengeti rrhaaaa raaaahhh.

No comments:

Post a Comment