Thursday, 30 December 2010

CHENGE AHUKUMIWA FAINI YA LAKI 7 LEO TU !

Mbunge wa Bariadi Magharibi na Waziri wa Miundombinu wa Serikali ya

awamu ya tatu Andrew Chenge, amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela

au faini ya Sh 700,000 na Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni ambapo

aliwasilisha faini hiyo mara baada ya hukumu hiyo kutolewa leo

asubuhi.

Akitoa hukumu hiyo jana Hakimu Mfawidhi aliyekuwa anasikiliza kesi

hiyo Kwey Rusema alisema uamuzi huo wa Mahakama unafuatia kukamilika

kwa ushahidi uliotolewa na mashahidi wa pande zote mbili katika kesi

hiyo iliyodumu kwa zaidi ya mwaka mmoja na miezi minane.

Akisoma ushahidi wa awali Rusema alisema Chenge anashitakiwa kwa

makosa manne yakiwamo kuendesha gari bila uangalifu, kusababisha vifo

vya wanawake wawili ambao ni Beatrice Costantine na Victoria Geogre,

kuendesha gari kwa uzembe na kuharibu pikipiki aina ya bajaj pamoja na

kuendesha gari lilikuwa na bima iliyokwisha muda wake.

Katika ushahidi wa awali Chenge aliukana na upande wa mashitaka ambapo

waliitwa mashahidi sita kati yao wanne walikuwa Askari Polisi akiwamo

Mrakibu Mwandamizi wa Polisi Fortunatus Musilimu.

Ushahidi uliotolewa mahakamani hapo ulidai tarehe 26 Machi 2009 majira

ya usiku wa manane Chenge akiwa katika matembezi yake binafsi alikuwa

anaendesha gari lake aina ya Toyota Hilux lenye namba za usajili

T512ACE kwenye barabara ya Haille Selasie Oysterbay jijini Dar es

Salaam aligonga bajaj na kusababisha ajali iliyosababisha vifo vya

wanawake wawili.

Maelezo yaliyotolewa mahakamani hapo kuhusu kuendesha gari kwa uzembe

na kuharibu bajaj Chenge aliyakana na kwa madai kuwa alikuwa katika

mwendo wa kawaida kati ya kilo mita 30 hadi 50 na kudai kuwa dereva wa

bajaj alimfuata upande wake kwani yeye alikuwa upande wa kulia zaidi.

Hukumu hiyo ambayo ilitakiwa kusomwa Desemba 16, mwaka huu,

iliahirishwa baada ya Hakimu kukubali ombi la Wakili wa Chenge

aliyeomba kuahirishwa kwa hukumu hiyo kwa kuwa mteja wake alipata

udhuru.

Mponda alidai kuwa mshitakiwa asingeweza kufika mahakamani hapo kwa

kuwa alisafiri kwenda Mwanza kwenye msiba na kuiomba Mahakama

kuahirisha hukumu hiyo.
Kwa mara ya kwanza, Chenge alifikishwa mahakamani hapo Machi 28, 2009

akikabiliwa na mashitaka matatu likiwamo la kuendesha gari kwa uzembe

na kusababisha vifo vya wanawake wawili, kuharibu pikipiki ya matairi

matatu pamoja na kuendesha gari lisilokuwa na stika ya bima.

Katika ushahidi wake mahakamani hapo, Chenge ambaye ni Mbunge wa

Bariadi Magharibi, alidai kuwa shahidi wa tatu wa upande wa mashitaka,

Fortunatus Musilimu, ana ugomvi naye.

Chenge alidai shahidi huyo ambaye aliwahi kutoa ushahidi kuwa mabaki

ya ubongo wa marehemu yalikutwa kwenye gari la Chenge na kuwa

aliwasilisha bima batili, kuwa ni mwongo na ana ugomvi naye.

Ilidaiwa kuwa Machi 27, mwaka jana katika Barabara ya Haile Selassie

Oysterbay, Chenge akiendesha gari aina ya Toyota Hilux Pick Up lenye

namba za usajili T512 ACE, aliigonga pikipiki ya matairi matatu

(bajaj) yenye namba T736 AXC na kusababisha vifo vya Beatrice

Costantino na Vick George.

No comments:

Post a Comment