Saturday, 7 November 2009

HISTORIA FUPI YA MAREHEMU ALEX MUKAMA KUSSAGA




Kuzaliwa; Marehemu alizaliwa Julai 7, 1932 katika kijiji cha Bwasi Majita Musoma vijijini.

Masomo;


= Elimu ya Msingi alisoma Bukima Primary school kuanzia mwaka 1942 ambapo alihitimu darasa la nne. Mwaka 1946 alijiunga na Shule ya Mwisenge Middle school ambapo alisoma darasa la tano hadi la nane.



= Mwaka 1951 alijiunga na Chuo cha Ualimu Pasiansi Mwanza na kufuzu cheti cha Ualimu mwaka 1952.

= Mwishoni mwa mwaka 1952 baada ya kuhitimu cheti cha Ualimu alibakizwa hapo chuoni kama mkufunzi. Aliendelea kufundisha Pasiansi Teacher Training Centre hadi chuo kilipohamishiwa Butimba Teacher Training Centre-Mwanza. Alijiuzulu kazi ya ualimu mwaka 1959 na kujiunga na vyama vya Ushirika Ukerewe Growers Corperative Union.

= Mwaka 1961 aliacha kazi ya Ushirika na kuingia Serikali kuu ambapo alipelekwa Mzumbe Institute of administration kusomea utawala. Baada ya kumaliza masomo Mzumbe 1962 aliteuliwa kuwa Local Government Officer kule Njombe District-Southern Highlands Province wakati huo.

= Kwa juhudi na bidii aliyokuwa nayo kazini, mwaka 1964 alipandishwa cheo kuwa Regional Local Government Officer-Southern Highlands Province-Mbeya.

= Mwaka 1965 alihamishiwa Musoma na kuteuliwa kuwa Town Clerk wa mji wa Musoma.

= Mwaka 1967 alihamishiwa mjini Iringa kama Town Clerk, mji ambao ulikuwa mkubwa kuliko Musoma.

= Mwaka 1968 alipandishwa cheo na kuhamishiwa Mwanza kama Town Clerk ambako alifanya kazi hadi mwanzoni mwa mwaka 1973 ambapo alihamishiwa Mtwara Township.


= Akiwa Mtwara, marehemu alijiuzulu kazi za Serikali na kujiunga na Shirika la Bima la Taifa kama Meneja Utawala mwaka 1973 april. Akiwa Meneja utawala Bima, mwaka 1976 alikwenda Uingereza kuchukua mafunzo ya Utawala katika Chuo kikuu cha Manchester.Aliendelea kufanya kazi Bima na kupandishwa cheo kufikia ngazi ya Mkurugenzi wa Utawala Shirika la Bima hadi alipostaafu 1991.


Mzee Alex alishiriki katika uundwaji wa kampuni kubwa ya Media inayoitwa Clouds Entertainment. Kampuni hii ikihodhi baadhi ya makampuni yafuatayo; Clouds fm/choice fm/clouds tv ambapo mpaka kutokea kifo chake yeye akiwa ndiye Mwenyekiti.

Marehemu ameacha mke na watoto tisa, pamoja na wajukuu 11.
Mungu alitoa na Mungu ametwaa, jina la Bwana lihimidiwe
, Amen.

Mwili wa marehemu Alex Kusaga ukitolewa kanisani kwa ajili ya kwenda kuzikwa katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar
Mkurugenzi wa Clouds Media Gropu/Prime Time Promotions Joseph Kusaga pamoja na familia yake akitoa heshima za mwisho kwa baba yake mzee Alex Kusaga mchana huu katika kanisa la Azania Front,jijini Dar
Rais mstaafu wa awamu ya tatu ,Mh Benjamin Mkapa akitoa heshima za mwisho mbele ya mwili wa marehemu mzee Alex Kusaga mchana huu katika kanisa la Azania Front,jijini Dar.
Mama Anna Mkapa akitoa heshima za mwisho mbele ya mwili wa marehemu Mzee Alex Kusaga
Mke wa marehemu akitoa heshima za mwisho mchana huu ndani ya kanisa la Azania Front
watoto wa marehemu mzee Alex Kusaga wakitoa heshima za mwisho mchana huu kanisani
wakati wa sala,kulia ni Rais mstaafu wa awamu ya tatu,Mh William Benjamini Mkapa na mkewe Mama Anna MKapa
Rais mstaafu wa awamu ya tatu,Mh William Benjamini Mkapa na mkewe Mama Anna MKapa na Mke wa Marehemu wakisoma kitabu cha sala

Familia ya marehemu,Mzeee Alex Kusaga wakiwa katika majonzi baada ya kuondokewa mpendwa wao,pichani wakisikiliza kwa makini sala iliyokuwa ikiendeshwa kwa ajili ya kumuombea marehu.

Ngugu wa marehemu Mzee Alex Kusaga wakiwa kanisani le mchana

Baadhi ya ndugu jamaa na marafiki wakiwa wametulia kwa makini wakifuatilia sala iliyokuwa ikiendeshwa kwa ajili ya kumuombea marehemu,Mzee Alex Kusaga.
Ndugu,jamaa na marafiki walifika kwa wingi kanisani kwa ajili kutoa heshima zao za mwisho kwa mpendwa wao Marehemu Alex Kusaga.
Baadhi ya wafanyakazi wa Clouds Fm/Tv wakiwa wametulia tulii wakifuatilia yaliyokuwa yanajiri ndani ya kanisa leo mchana.
Akina mama wakiwa katika nyuso za huzuni leo mchana nje ya kanisa la Azania Front baada ya kuondokewa mpendwa wao Mzee Alex Kusaga.
Mwili wa marehemu ukiwekwa kwa makini
Mwili wa marehemu Mzee Alex Kusaga ukiwasili kanisani leo mchana katika kanisa la Azania Fron,jijini Dar na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa watu.

No comments:

Post a Comment